JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI
021KISWAHILI
Muda: 2:30 Mwaka: 2025
Maelekezo
Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10).
Jibu maswali yote kwenye nafasi ulizopewa.
Sehemu A na C zina alama kumi na tano (15) kila moja na sehemu B ina alama sabini (70).
Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhiusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji.
Andika Namba yako ya Upimaji katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.
KWA MATUMIZI YA MPIMAJI TU
NAMBA YA SWALI
ALAMA
SAHIHI YA MPIMAJI
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
JUMLA
SAHIHI YA MHAKIKI
SEHEMU A (Alama 15)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Katika vipengele (i) - (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kisanduku ulichopewa.
(i) Mpangilio sahihi wa maneno yafuatayo katika kamusi ni upi?
Shaba, shadidi, shahada, shamba, shangazi
Shaba, shahada, shangazi, shamba, shadidi
Shaba, shangazi, shamba, shadidi, shahada
Shaba, shamba, shangazi, shadidi, shahada
Choose Answer :
(ii) Mwalimu alitufundisha kuwa mizani ni kipengele muhimu cha fani katika ushairi wa fasihi simulizi. Ipi ni maana sahihi ya kipengele hicho?
Silabi au sauti zenye milio ya kufanana katika ubeti
Mstari mzima wa shairi unaojitosheleza kimaana
Mshororo wa mwisho wa kila ubeti wa ushairi
Idadi ya silabi katika mshororo au mstari wa shairi
Choose Answer :
(iii) "Wanafunzi hawapendagi somo la Hisabati kwa kuwa ni gumu." Kosa la kisarufi lililopo katika sentensi hiyo limesababishwa na nini?
Kutozingatia alama za uandishi
Uongezaji wa kiambishi
Udondoshaji wa herufi
Upatanisho wa kisarufi
Choose Answer :
(iv) Sentensi ipi imejengwa na kauli ya kutendewa?
Shamba limelimika lote
Kitabu kimechanika
Mafuta yameisha kabisa
Nyumba imejengewa ua
Choose Answer :
(v) Miundo ya barua ya kindugu na rasmi hutofautishwa na jambo lipi?
Anwani ya mwandishi
Tarehe ya barua
Anwani ya mwandikiwa
Jina la mwandishi
Choose Answer :
(vi) Sentensi ipi si sahihi kuhusu sifa za fasihi simulizi?
Huwasilishwa kwa mdomo
Huwa ni mali ya jamii nzima
Hubadilika kulingana na wakati
Humilikiwa na mwandishi
Choose Answer :
(vii) Sentensi ipi haina kielezi cha mahali?
Anasoma kwa bidii
Anapikia chai jikoni
Anachezea uwanjani
Dereva ameingia barabarani
Choose Answer :
(viii) Nyenzo kuu ya ufahamu wa kusikiliza ni ipi?
Kusoma matini kwa makini
Kutambua aina ya matini
Kusikiliza matini kwa makini
Kujibu maswali kwa makini
Choose Answer :
(ix) Maelezo yapi yanabainisha udhaifu wa kuhifadhi kazi za fasihi simulizi kwa njia ya kichwa?
Haihitaji gharama
Huwasilishwa popote
Humilikiwa na hadhira
Hupotea kwa urahisi
Choose Answer :
(x) Sehemu ya neno inayoundwa na konsonanti na irabu au irabu peke yake na hutamkwa kwa pamoja kama fungu moja la sauti huitwaje?
Sauti
Silabi
Neno
Sentensi
Choose Answer :
2. Oanisha viambishi vilivyopigiwa mstari katika Orodha A na dhima ya kiambishi husika kutoka Orodha B kisha andika jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa.
3. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Wananchi wa Tanzania tunalo jukumu kubwa la kulijenga taifa letu. Tukumbuke kuwa tunapolijenga taifa letu tunawajenga watu wake, kwa kuwa taifa ni jumuiya ya watu. Kuna njia moja muhimu inayoweza kutumika ili kuwafanya watu wajiletee maendeleo yao wenyewe ambayo ni kuelekezwa na kuzingatia maelekezo sahihi ya viongozi wao. Uongozi wa jambo lolote huzingatia kuzungumza na kushauriana na watu, kuwaeleza na kuwashawishi.
Katika nchi ya Tanzania, mazungumzo, ushauri, maelekezo na vishawishi baina ya viongozi na watu katika kuleta maendeleo na kulijenga taifa yanafanyika kwa kutumia lugha ya Kiswahili. Lugha ya Kiswahili kwa hivi sasa kimekuwa chombo adhimu kinachotuwezesha kupeana maelekezo na kutoa mrejesho wa maelekezo yaliyotolewa.
Kiswahili kimekuwa mstari wa mbele katika kazi kubwa ya kulijenga taifa letu. Ili kazi hii ifanikiwe yatubidi wananchi wote wa Tanzania tujifunze Kiswahili, tukiheshimu na tukitumie katika shughuli zetu zote. Ikiwa tutakibeza na kuamua kwamba kila mmoja wetu ashikilie lugha ya kabila lake, basi yatatukumba matatizo ya ukabila.
Tuangalie nasi tusije tukashindwa kuendelea kujenga nchi yetu kwa sababu ya kukosa maelewano. Kama hatuna lugha ya kutuunganisha tutashindwa kutekeleza majukumu tunayopewa na viongozi wetu, ukiwemo utii wa sheria na kutimiza mipango mbalimbali. Kukosa maendeleo si shabaha yetu, hivyo, jambo kubwa la kwanza yatupasa tufahamu kwamba Kiswahili ndiyo lugha ya taifa tusifanye ajizi tunapaswa kuitumia.
Maswali
(a) Andika kichwa cha habari uliyosoma kwa maneno yasiyozidi matano.
(b) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika habari uliyoisoma:
Adhimu
Tutakibeza
Yatatukumba
Ajizi
(c) Ni njia ipi inashauriwa kutumika katika kuwaletea watu maendeleo?
(d) Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 50 na yasiyozidi 60.
Jembe wangu nakuhitaji, uje unipe neema, Jembe wewe ndiwe chaji, twakuenzi tangu zama, Jembe wewe ni mpaji, wa baba na hata mama, Jembe ndiwe mkombozi, tangu enzi za wahenga.
10. Wewe ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Chajjaba S.L.P 207, Morogoro na unatarajia kufanya kazi ya kuuza magazeti katika likizo yako ya Desemba mwaka huu. Andika barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa gazeti la Nipashe, S.L.P 1012, Dar es Salaam kuomba kazi hiyo. Jina lako liwe Shukuru Maarifa.